Jumamosi, 6 Septemba 2014

NGUO ZA MITUMBA NI HATARI SANA HEBU ONA HAPO CHINI

Hao unaowaona kama weusi weusi kwenye ziwa hapo ni funza ambao wameform matobo matobo ambapo wanatoka nje sasa baada ya kukomaa ki ukweli tunatakiwa tuwe makini sana na nguo hizi za mitumba tunatakiwa tuzifue kwa maji ya moto ili kuua vimelea na madawa yaliyopuliziwa vinginevyo tutaumia sana na hii pia ni fundisho kwa wale wenye kuvaa nguo za ndani za mitumba pia bila kuzifua wadada na wakaka tuweni makini kwenye mavazi yetu ukiona ujumbe huu mtaarifu na mwenzio auone SHARE kwa manufaa ya wengine. Asanten

Alhamisi, 27 Februari 2014

SISI NA KATIBA MPYA

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema (kushoto), akizungumza na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda kabla ya kuanza kikao cha Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma jana. Picha:Selemani Mpochi.

 

Mwenyekiti Bunge la Katiba nguvu kwa Migiro,Chikawe


  Yadaiwa ni baada ya mambo kumemwendea vibaya Chenge
Waziri wa Katiba na Sheria,Dk. Asha-Rose Migiro.
Kampeni  za makundi ya vigogo wanaopigana vikumbo kugombea uenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba zimechukua sura mpya, baada ya kundi lililokuwa likimuunga mkono Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge kudaiwa kubadili ghafla mwelekeo wa kampeni zake.

 Habari za kuaminika zilizopatikana mjini hapa jana zilieleza kuwa kundi hilo lililokuwa likimtaka Chenge, sasa linataka nafasi hiyo iwaniwe na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro au Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe.

 Hatua hiyo inadaiwa kuchukuliwa na kundi hilo baada ya kubaini kuongezeka kila uchao kwa nguvu za Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye tayari ameshatangaza kuwania nafasi hiyo, huku zile walizozitarajia kutoka kwa Chenge zikizidi kushuka.

 Habari hizo zinaeleza kuwa uthibitisho wa hilo, ni ujasiri ulioonyeshwa na Sitta aliyeamua kutangaza hadharani azma yake ya kuwania nafasi hiyo, huku Chenge akishindwa kuthibitisha kuwa atagombea ama la.

Uchaguzi wa mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba unatarajiwa kufanyika Jumapili wiki hii baada ya Bunge hilo kupitisha azimio la kuipitisha rasimu ya kanuni za Bunge Maalumu kesho.

Awali, Chenge aliiambia NIPASHE kuwa hayuko tayari kutangaza kama atagombea nafasi hiyo au la kwa kuwa kanuni za Bunge hilo bado hazijatungwa.

Kauli kama hiyo iliwahi pia kutolewa na Waziri Sitta katika siku hiyo hiyo, ambayo Chenge aliashiria kusubiri kanuni.

Hata hivyo, siku chache baadaye, hata kabla ya rasimu ya kanuni hizo haijapitishwa na Bunge, Waziri Sitta alitangaza azma yake ya kugombea nafasi hiyo kwa maelezo kwamba, anataka kutimiza ndoto ya Rais Jakaya Kikwete ya kupata katiba bora.

Jumatatu wiki hii, Chenge alipoulizwa na NIPASHE kuhusiana kinyang'anyiro hicho, alikataa kuzungumza na badala yake akamtaka mwandishi aendelee na shughuli zake.

Waziri Chikawe alipotafutwa na NIPASHE jana kuzungumza kama ana nia ya kugombea nafasi hiyo au la, alimtaka mwandishi kuvuta subira kwa kuwa wakati huo hakuwa na nafasi ya kuzungumza.

Dk. Migiro ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa (UN) hakupatikana
kuzungumzia suala hilo.

Jitihada za kuwatafuta viongozi hao wanaotajwa kuwania nafasi hiyo zinaendelea.
CHANZO: NIPASHE